sw_tn/isa/05/01.md

1.0 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anasema fumbo juu ya mkulima na shamba lake la mizabibu. Mkulima anawakilisha Mungu na shamba la mizabibu linawakilisha watu wa Yuda, ufalme wa kusini wa Waisraeli.

ninayempenda

"rafiki yangu kipenzi"

juu ya kilima chenye rutuba

"juu ya kilima ambapo mazao mazuri yanaweza kuota"

akachimbua kwa sepeto

"Ameandaa udongo". Msemo huu una maana ya kutumia kifaa kuchimba katika ardhi kuiandaa kwa ajilii ya kupanda.

Akajenga mnara katikati yake

"Alitengeneza jengo refu katikati ya shamba la mizabibu kuutazama". Mtu alikuwa akisimama juu ya mnara kutazama shamba la mizabibu na kuhakikisha hakuna wanyama au watu watakaoingia ndani mwake. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

kujenga kishinikizo cha zabibu

"alichimba shimo kuminya juisi ya zabibu". Kishinikizo cha zabibu ni sehemu ya chini iliyochongwa kwa jiwe katika ardhi ambapo wafanyakazi hukanyaga juu ya zabibu kuisaga kwa miguu yao, ili kutoa juisi ya zabibu.

zabibu mwitu

"zabibu zisizo na thamani" au "zabibu zenye ladha mbaya"