sw_tn/isa/04/03.md

1.6 KiB

yule ambaye amebaki Sayuni na yule ambaye anabaki Yerusalemu

Kauli hizi mbili zina maana moja. Hapa "yule ambaye" haimaanishi mtu dhahiri lakini watu kwa ujumla ambao bado wako hai Yerusalemu. "kila mtu ambaye anabaki Yerusalemu"

ataitwa mtakatifu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Bwana atawaita watakatifu" au "watakuwa wa Bwana"

kila mmoja ambaye ameandikwa chini kama aishiye Yerusalemu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kila mmoja ambaye jina lake lipo katika orodha ya watu ambao wanaishi Yerusalemu"

Bwana atakapokuwa ameosha uchafu wa binti wa Sayuni

Msemo huu unazungumzia dhambi kana kwamba ilikuwa uchafu halisi. "baada ya Bwana kuondoa dhambiu ya binti wa Sayuni kama vile mtu anavyoosha uchafu"

binti wa Sayuni

Maana zawezekana kuwa 1) wanawake wa Yerusalemu au 2) watu wa Yerusalemu

na atakuwa amesafisha madoa ya damu kutoka miongoni mwa Yerusalemu

"Madoa ya damu" hapa yanawakilisha vurugu na mauaji. "na atakuwa amewaondoa wale walioko Yerusalemu ambao huwadhuru watu wasio na hatia"

kwa njia ya roho wa hukumu na roho anayewaka moto

Hii ni jinsi Mungu atakavyotoa dhambi kutoka Yerusalemu. Hapa "roho" huenda inawakilisha tukio la kuhukumu na kuchoma. "kwa hukumu na moto unaowaka"

roho wa hukumu

Maana zawezekana kuwa 1) Yahwe atawaadhibu watu au 2) Yahwe atawatangaza kuwa na hatia

roho awa moto uwakao

Maana zawezekana kuwa 1) hii ni sitiari ambayo inamaanisha Yahwe ataondoa wenye dhambi kutoka Sayuni kama moto uondoavyo uchafu au 2) "moto unaowaka" ni mfano wa maneno yanayowakilisha uharibifu kwa ujumla wa wenye dhambi wote.