sw_tn/isa/02/20.md

1.4 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi. Anaendelea kufafanua kile kitakachotokea katika siku ya Yahwe wa Majeshi.

kwa fuko na popo

Fuko ni wanyama wadogo ambao huchimba na kuishi chini ya ardhi. Popo ni wanyama wanaopaa wadogo ambao mara nyingi huishi ndani ya mapango. "kwa wanyama"

mianya katika mawe .. nyufa za mawe yaliyopasuka

Kama lugha yako haina maneno mawili tofauti kwa ajili ya "mianya" na "nyufa", nafasi inayojitokeza katikati ya sehemu mbili ya jiwe linapogawanyika, unaweza kuunganisha misemo hii miwili kuwa moja.

kutoka kwa hofu kuu ya Yahwe

kwa sababu walikuwa wakuimuogopa sana Yahwe.

utukufu wa ukuu wake wa enzi

"uzuri wake mkuu na nguvu ambayo anayo kama mfalme" au "ukuu wake wa enzi wa kifalme"

atakapoinuka kutisha dunia

"pale Yahwe anapochukua hatua na kusababisha watu wa dunia kumuogopa sana"

ambaye pumzi yake ya uhai ipo katika pua zake

pumzi ipo ndani ya pua zake Pua ni dhaifu na shimo za pua ni nzuri, kwa hiyo pia ni mfano wa watu, ambao ni dhaifu. "ni nani ambaye ni dhaifu na atakufa" au "nani anahitaji pumzi katika pua yake kuishi"

pua

mashimo katika pua ambapo watu hupumulia

kwa maana ataambulia wapi?

Isaya anatumia swali kuwakumbusha watu kitu ambacho wanapaswa kuwa wanakijua tayari. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "kwa maana mtu ataambulia patupu!" au "kwa maana mtu hana faida yoyote!"