sw_tn/isa/02/14.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi. Anaendelea kufafanua kile kitakachotokea katika siku ya Yahwe wa Majeshi.

na dhidi ya

Katika 2:14-16 Isaya anaorodhesha viitu ambavyo Mungu ataangamiza. Maana zaweza kuwa 1) hivi vina maana ya watu wenye kiburi ambao Mungu atawashusha au 2) Mungu atawaangamiza kabisa vitu hivi katika orodha.

milima ... vilima

Maneno haya ni sitiari kwa ajilii kiburi cha Waisraeliu. Pia zinajitokeza katika 2:1.

ambayo imeinuliwa juu

Hii ni lahaja. "ambayo iko juu sana"

mnara wa juu ... ukuta usioshindika

Hii ina maana ya vitu ambavyo watu watajenga kuzunguka miji yao ilii waweze kujilinda dhidi ya adui zao. Ni sitiari kwa ajili ya kiburi cha Waisraeli na waliamini hawakuwa na hitaji la Yahwe na wangeweza kusimama dhidi ya adhabu yoyote Yahwe angewapimia kwao kwa ajili ya dhambi zao.

ukuta usioshindika

"ukuta ambao hakuna kitu kinachoweza kuvunja au kupita katikati"

meli za Tarshishi ... vyombo vizuri vya matanga

Hizi zina maana ya meli kubwa ambazo watu walitumia kusafiri mbali juu ya bahari na kuleta bidhaa katika miji yao.

meli za Tarshishi

"meli ambazo wanatumia kwenda Tarshishi"