sw_tn/isa/02/12.md

1010 B

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

ambaye ana kiburi na ameinuliwa

Yule ambaye "ameinuliwa" ana majivuno na kujichukulia kuwa bora kuliko watu wengine. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambaye anajisifu na anajiinua juu ya watu wengine" au "ambaye anajivuna na kufikiri ya kwamba yuko bora kuliko watu wengine"

ambaye ana kiburi ... ambaye anajisifa

Mtu ambaye ana majivuno anaongeza na kutenda kana kwamba yupo bora kuliko watu wengine. Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kusisitiza ya kwamba Yahwe atawaadhibu wao"

na yeye atashushwa chini

"na kila mtu mwenye kiburi atashushwa chini". Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atamnyenyekeza"

dhidi ya mierezi ya Lebanoni ... dhidi ya mwaloni ya Bashani

"Siku ya Yahwe wa Majeshi" itakuwa dhidi ya mierezi na mwaloni. Maana zaweza kuwa 1) miti hii ni sitiari kwa watu wenye kiburi ambao Mungu atawahukumu au 2) Mungu kwa uhakika ataangamiza miti hii mikuu.