sw_tn/isa/02/09.md

2.2 KiB

Taarifa ya Jumla

Katika 2:9 Isaya anamaliza kuzungumza na Yahwe. Katika 2:10-11 Isaya anazungumza na watu wa Yuda. Nyakati mbili anazungumza katika mtindo wa shairi.

Watu watainamishwa, na kila mtu binafsi ataanguka chini

Hapa kuwa chini mpaka ardhini inawakilisha watu ambao wameaibishwa kabisa kwa sababu wamegundua yote waliyoamini hayana maana, na hawawezi kufanya kitu kujisaidia wenyewe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "'Mungu atafanya watu waaibike, na watagundua ya kwamba waliamini katika vitu visivyo na maana"

Watu

binadamu, tofauti na wanyama

mtu binafsi

"kila mtu"

usiwainue juu

Maneno "kuwainua juu" ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kusamehe watu. "usiwasamehe"

Nenda katika sehemu za mawe

Maana zaweza kuwa watu wanapaswa kwenda katika 1) mapango juu ya teremko za upande wa milima au 2) sehemu ambapo kuna mawe makubwa mengi ambapo mtu atajificha.

jifiche katika ardhi

Maana zaweza kuwa ya kwamba watu wanapaswa kujificha 1) katika shimo la kawaida katika ardhi au 2) katika shimo ambalo wanachimba katika ardhi.

kutoka kwa hofu kuu ya Yahwe

Hapa nomino dhahania "hofu kuu" inaweza kuelezwa na kitenzi "kuogofya". "kutoka kwa uwepo wa kuogofya wa Yahwe" au "Kutoka kwa Yahwe kwa sababu utamwogopa sana"

utukufu wa ufalme wake

"uzuri wake mkuu na nguvu ambayo anayo kama mfalme" au "ufahari wake wa kifalme"

mtazamo wa kiburi wa mwanamume kutashushwa chini

"Yahwe atashusha chini mtazamo wa kiburi wa mwanamume". Mwanamume mwenye "mtazamo wa kiburi" anatazama juu ya kila mtu kuwaonyesha ya kwamba ni bora kuliko wao. Hapa watu wote wana hatia ya kufikiri wapo bora kuliko Yahwe, na jinsi wanavyotazama wale wanaomwabudu Yahwe, ni mfano wa maneno wa kiburi chao. "Yahwe atawaibisha watu wote kwa sababu wanafikiri wako bora kuliko yeye"

kiburi cha wanamume kutashushwa chini

Yahwe atawafanya wanamume wenye kiburi kuaibiika wao wenyewe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atashusha chini kiburi cha wanamume" "Wanamume wenye kiburi" ni mfano wa maneno wa watu wenye kiburi. "Yahwe atawashusha chini watu wenye kiburi"

Yahwe peke yake atainuliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watamsifu Yahwe tu"

katika siku hiyo

Hii ni lahaja. "katika siku ambayo Yahwe anahukumu kila mtu"