sw_tn/isa/02/03.md

1.4 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Yakobo, ili aweze kufundisha ... na tuweze kutembea

Maana nyingine ni "Yakobo . Atafundisha ... na tutatembea"

aweze kutufundisha baadhi ya njia zake, na tuweze kutembea katika njia zake

Neno "njia" ni sitiari kwa namna mtu anavyoishi. Kama lugha yako ina neno moja tu kwa ardhi ambayo watu wanatembea, unaweza kunganisha miseo hii miwili. "aweze kutufundisha mapenzi yake ili kwamba tuweze kumtii"

Kwa maana kutoka kwa Sayuni sheria itakwenda, na neno la Yahwe kutoka Yerusalemu

Misemo hii ina maana ya kitu kiimoja. Isaya alikuwa akisisitiza ya kwamba mataia yote yataelewa ya kwamba ukweli unapatikana Yerusalemu. "Watu wa Sayuni watafundisha sheria ya Mungu, na watu wa Yerusalemu watafundisha neno la Yahwe"

Kwa maana kutoka kwa Sayuni sheria itakwenda

"Kwa maana sheria itakwenda kutoka Sayuni". Isaya anazungumza kana kwamba sheria ilikuwa kitu kama mto ambao husogea bila watu kufanya lolote. "Wale ambao wanafundishwa sheria watatoka nje kutoka Sayuni" au "Yahwe atatangaza sheria yake kutoka Sayuni"

neno la Yahwe kutoka Yerusalemu

"neno la Yahwe litatoka kutoka Yerusalemu". Isaya anazungumza kana kwamba neno la Yahwe lilikuwa kitu kama mto ambacho kinasogea bila watu kufanya lolote. Unaweza kufanya taarifa inayoeleweka wazi. "Wale ambao wanafundishwa sheria watatoka nje kutoka Yerusalemu" au "Yahwe atatangaza sheria yake kutoka Yerusalemu"