sw_tn/isa/01/21.md

1.5 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Jinsi mji mwaminifu

Neno hili la mshangao linaonyesha hasira na huzuni ya Isaya juu ya watu wa Yerusalemu. "Tazama jinsi watu wa Yerusalemu, ambao wamekuwa waaminiufu kwa Mungu"

ulivyokuwa kahaba

Isaya analinganisha watu na mwanamke ambaye sio mwaminifu kwa mumewe lakini analala na wanamume wengine kwa pesa. Watu hawakuwa waaminifu kwa Mungu lakini walikuwa wakiabudu miungu ya uongo. "kutenda kama kahaba"

Alikuwa amejaa haki

Neno "alikuwa" ina maana ya Yerusalemu na watu wake. Wale waliondika Biblia mara kwa mara walimaanisha miji kama wanawake. "Watu wa Yerusalemu walikuwa wa haki na walifanya kilicho sahihi"

lakini sasa amejaa wauaji

Neno "amejaa" lina maana ya Yerusalemu na watu wake. Wale waliondika Biblia mara kwa mara walimaanisha miji kama wanawake. "lakini sasa watu wa Yerusalemu ni wauaji"

Fedha yako imekuwa chafu, divai yako imechanganywa na maji

Maana zawekekana kuwa ya kwamba Isaya anatumia fedha na divai kama sitiari ya 1) watu wa Yerusalemu. "Wewe ni kama fedha ambayo sio safi tena, na kama divai ambayo imechanganywa na maji" au 2) matendo mema ambayo watu walifanya awali. "Mlikuwa mkifanya matendo mema, lakini sasa matendo yenu mabaya yanafanya matendo yenu mema kutokuwa na maana".

fedha ... chafu

Mtu huhitaji kusafisha fedha mara kwa mara au haitang'aa tena.

divai ... maji

Divai na maji ndani yake ina ladha kidogo na kwa hiyo haitofautiani na maji.