sw_tn/isa/01/16.md

988 B

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Jioshe, jisafishe

Hapa Mungu analinganisha mtu anayeacha kutenda dhambi na mtu ambaye anaosha mwili wake. "Tubu na uoshe dhambi kutoka moyoni mwako kama uanvyoosha uchafu kutoka mwilini mwako"

ondoa uovu wa matendo yako kutoka machoni pangu

Mungu hakuwa anawaambia kufanya matendo yao maovu sehemu nyingine, lakini kuacha kuyafanya. "acha kufanya matendo maovu ambayo naona mnafanya"

nyosha wima ukandamizaji

Mungu anazungumza na watu ambao huwakandamiza wengine kana kwamba wamefanya kitu kupinda ambacho kilitakiwa kuwa wima, na anawaita kukifanya kitu hicho kuwa wima tena. Nomino dhahania "ukandamizaji" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "hakikisha ya kwamba wale watu wasiojiweza uliowadhuru hawateseki kutoka na mambo mabaya uliyofanya kwao"

toa haki kwa yatima

"uwe na haki kwa watoto ambao hawana baba"

walinde wajane

"walinde wanawake ambao waume zao wamefariki"