sw_tn/isa/01/10.md

519 B

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

nyie watawala wa Sodoma ... nyie watu wa Gomora

Isaya analinganisha watu wa Yuda na Sodoma na Gomora kusisitiza jinsi walivyokuwa wenye dhambi. "nyie watawala ambao mna dhambi kama watu wa Sodoma ... nyie watu ambao ni waovu kama wale walioishi Gomora"

"Wingi wa sadaka zako kwangu ni upi?"

Mungu anatumia swali kukaripia watu. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Sadaka zako nyingi hazina maana yoyote kwangu!"