sw_tn/hos/09/07.md

753 B

Taarifa ya julma:

Nabii Hosea anazungumza.

Siku za adhabu zinakuja; siku za kulipiza kisasi zinakuja

Hosea amesema kitu kile kile ili kusisitiza kuwa Bwana anakuja kuwahukumu watu wa Israeli kwa matendo yao maovu.

Nabii ni mpumbavu, na mtu aliyevuviwa ni mwendawazimu

Sentensi hii yaweza kuwa na maana 1) watu waliwaona manaabii kama wapumbavu au 2) manabii walichanganyikiwa kwa sababu ya dhambi zilizofanywa na watu.

Nabii ni mpumbavu, na mtu aliyevuviwa ni mwendawazimu

"nabii" na "mtu aliyevuviwa" zote zinamaanisha ni mtu anayesema kuwa amepokea ujumbe kutoka kwa Mungu.

kwa sababu ya uovu wako mkubwa na uadui mkubwa

"uovu mkubwa" na "uadui mkubwa" vina maana moja. Uovu wa watu unapelekea uadui dhidi ya Bwana na manabii wake.