sw_tn/gen/50/15.md

1.5 KiB

Itakuwaje ikiwa Yusufu atatukasirikia

Hapa hasira inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu cha kimwili ambacho Yusufu alikishika kwa mkono wake. "Je iwapo Yusufu atakuwa bado na hasira na sisi"

akataka kutulipa kikamilifu kwa ajili ya uovu tuliomtenda

Kulipiza mwenyewe dhidi ya mtu mwingine aliyemdhuru inazungumziwa kana kwamba mtu alikuwa akilipa mtu mwingine kile walichodai. "anataka kulipiza kwa uovu tuliofanya kwake"

Baba yako alitoa maelekezo kabla hajafa, kusema, 'Mwambieni hivi Yusufu, "Tafadhali samehe makosa ya ndugu zako na dhambi yao uovu waliokutenda."

Hii ina madaraja mawili ya nukuu na madaraja matatu ya nukuu. Zinaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Baba yako alituagiza kabla ya kufa tukuambie ya kwamba utusamehe kwa uovu tuliokufanyia kwako"

Baba yako alitoa maelekezo kabla hajafa, kusema

Yakobo alikuwa baba wa ndugu wote. Hapa wanasema "baba yako" kusisitiza ya kwamba Yusufu anahitaji kuvuta nadhari kwa kile baba yake alichosema. "Kabla baba yetu hajafa alisema"

na dhambi yao uovu waliokutenda

"kwa mambo maovu waliyokufanyia kwako"

Basi

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Basi wasamehe watumishi wa Mungu wa baba yako

Ndugu wanajitambulisha kama "watumishi wa Mungu wa baba yako". Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "tafadhali tusamehe, watumishi wa Mungu wa baba yetu"

Yusufu akalia walipomwambia.

"Yusufu alilia aliposikia ujumbe huu"