sw_tn/gen/50/04.md

1.5 KiB

Siku za maombolezo

"siku za kumuomboleza" au "siku za kumlilia"

Yusufu akaongea na watumishi wa baraza la kifalme

Hapa "baraza la kifalme" ina maana ya maafisa ambao huunda baraza la kifalme la Farao. "Yusufu alizungumza na maafisa wa Farao"

Ikiwa nimepata kibali machoni penu

Msemo "machoni penu" ni lugha nyingine yenye maana ya fikra na mawazo ya Yakobo. "Iwapo nimepata kibali kwako" au "kama umefurahishwa na mimi"

nimepata kibali

Hii ni lahaja yenye maana ya kwamba mtu amekubalika na mtu mwingine.

tafadhali ongeeni na Farao, kusema, 5'Baba yangu aliniapisha, kusema, "Tazama, ninakaribia kufa. Unizike katika kaburi nililolichimba kwa ajili yangu mwenyewe katika nchi ya Kanaani. Ndipo utakaponizika." Basi sasa niruhusu niende nimzike baba yangu, na kisha nitarudi."

Hii ina madaraja mawili ya nukuu na madaraja matatu ya nukuu. Hizi zinaweza kuwekwa kama nukuu zisizo moja kwa moja. "tafadhali mwambie Farao ya kwamba baba yangu alinifanya niape ya kuwa baada ya kufa kwake nitamzika katika kaburi ambalo alilichimba kwa ajili yake katika nchi ya Kaanani. Tafadhali muombe Farao aniruhusu niende kumzika baba yangu, na kisha nitarudi.

Tazama, ninakaribia kufa

"Tazama, ninakufa"

niruhusu niende juu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kwenda juu" pale izungumzwapo safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Farao akajibu

Inasemekana ya kwamba wajumbe wa baraza walizungumza na Farao, na sasa Farao anamjibu Yusufu.

kama alivyokuwapisha

"kama ulivyoapa kwake"