sw_tn/gen/49/14.md

1.2 KiB

Isakari ni punda mwenye nguvu

Yakobo anazungumzia kuhusu Isakari na uzao wake kana kwamba walikuwa punda. Hii inasisitiza ya kwamba watafanya kazi kwa bidii. "Uzao wa Isakari utakuwa kama punda mwenye nguvu"

Isakari ni

Mara nyingi katika unabii matukio ambayo yatatokea baadae inaelezwa kama kitu ambacho tayari kinaendelea. Hii inasisitiza ya kwamba tukio litatokea hakika. Inaweza kuwekwa kwa lugha ya baade. "Isakari atakuwa" au "Uzao wa Isakari utakuwa"

Isakari ... Anaona ... Atainamisha

Hapa "Isakari" ni lugha nyingine yenye maana ya uzao wake. "Uzao wa Isakari ... Wanaona .. Wataona"

ajilazaye kati ya kondoo

Maana zaweza kuwa 1) "ajilazaye chini katikati ya kundi walizokuwa wakibeba" au 2) "ajilazaye chini katikati ya zizi la kondoo".Kwa namna yoyote ile, Yakobo anazungumzia kuhusu uzao wa Isakari kana kwamba walikuwa punda ambao wamefanya kazi kwa bidii na wamejilaza chini kupumzika.

mahali pazuri pa kupumzikia na nchi ya kupendeza

"sehemu ya kupumzikia ambayo ni nzuri na kwamba nchi inapendeza"

Atainamisha bega lake kwa mzigo

Msemo huu "Atainamisha bega lake kwa mzigo" ni njia ya kusema "fanya kazi kwa bidii kubeba mzigo"

kuwa mtumishi wake kwa kazi ile

"watafanya kazi kwa wengine kama watumwa"