sw_tn/gen/49/07.md

1.0 KiB

Hasira yao na ilaaniwe, kwani ilikuwa kali - na ukali wao, kwani ulikuwa ni katili

Mungu kumlaani Simoni na Lawi inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa akilaani hasira na ukali wao. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Bwana anasema, 'Nitawalaani kwa sababu ya hasira yao kali na ukali wao mkatili" au "Mimi, Bwana, nitawalaani kwa sababu ya hasira ya kali na ukali wao mkatili"

Hasira yao na ilaaniwe

Katika unabii, nabii mara nyingi huzungumza maneno ya Mungu kana kwamba Mungu mwenyenwe alikuwa akizungumza. Hii inasisitiza ukaribu ulivyo kati ya nabii na Mungu.

na ukali wao, kwani ulikuwa ni katili

Neno "nitalaani" linaeleweka. "nami nitalaani ukali wao, maana ulikuwa katili"

Nitawagawa katika Yakobo na kuwatawanya katika Israeli

Neno "Nitawagawa" lina maana ya Mungu. Neno "kuwatawanya" lina maana ya Simoni na Lawi lakini ni lugha nyingine yenye maana ya uzao wao. Maneno "Yakobo" na "Israeli" ni lugha nyingine yenye maana ya watu wote wa Israeli. "Nitawagawanya uzao wao na kuwasambaza miongoni mwa watu wote wa Israeli"