sw_tn/gen/45/19.md

953 B

Maelezo ya Jumla

Farao anaendelea kumwambia Yusufu kipi cha kuwaambia ndugu zake.

Basi

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

mmeamriwa, 'Fanyeni hivi, chukueni mikokoteni kutoka Misri kwa ajili ya watoto wenu na kwa ajili ya wake zenu. Mchukueni baba yenu na kuja. Msijari kuhusu mali zenu, kwani mema yote ya nchi ya Misri ni yenu

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "pia waambie kuchukua mikokoteni kutoka katika nchi ya Misri kwa ajili ya watoto na wake zao, na kumchukua baba yao aje hapa. Hawatakiwi kuwa na wasiwasi kuhusu kuleta mali zao, kwa maana nitawapatia mambo mazuri tuliyonayo ndani ya Misri"

mmeamriwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nami nakuamuru kuwaambia" au "pia waambie"

chukueni mikokoteni

"Mikokoteni" ni gari dogo la abiria na mizigo lenye magurudumu mawili au manne. Wanyama huvuta mikokoteni.