sw_tn/gen/44/27.md

1.3 KiB

Maelezo ya Jumla:

Yuda anaendeleza simulizi yake kwa Yusufu

akatuambia, 'Mnajua kwamba mke wangu alinizalia wana wawili. Na mmoja akatoka kwangu nami nikasema, "Bila shaka ameraruliwa vipande, na tangu hapo sijamwona." Nanyi mkimchukua huyu naye kutoka kwangu mabaya yanaweza kumpata, mtashusha mvi zangu kwa kaburini kwa huzuni.

Hii ina madaraja mawili na daraja la tatu la nukuu. Yanaweza kuwekwa kama nukuu zisikzokuwa moja kwa moja. "akatuambia ya kwamba tunafahamu ya kuwa mke wake, Raheli, alimzalia watoto wawili tu, na kwamba mmoja wao alitoweka na mnyama alimrarua vipande vipande, na hajamuona tangu siku hiyo, kisha tutamfanya afe kwa huzuni"

akatuambia

Hapa "akatuambia" haimjumlishi Yusufu.

Mnajua

Hapa "mnajua" ni wingi na ina maana ya wale ndugu.

ameraruliwa vipande

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mnyama pori alimrarua vipande vipande"

mabaya yanaweza kumpata

Jambo baya linalotokea kwa mtu inazungumziwa kana kwamba "baya" lilikuwa kitu ambacho husafiri na kuja kwa mtu.

mtashusha mvi zangu kwa kaburini kwa huzuni

"kushusha ... Kuzimu" ni njia ya kusema watasababisha afariki na kushuka Kuzimu. Anatumia neno "shuka" kwa sababu iliaminika Kuzimu ilikuwa sehemu ya chini. "kisha mtanisababisha, mtu mzee, kufa kwa huzuni"

mvi zangu

Hii ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "mimi, mtu mzee"