sw_tn/gen/44/23.md

1.7 KiB

Maelezoya jumla:

Yuda anaendelea simulizi yake kuhusu Yusufu.

Na ukawambia watumishi wako, 'Mdogo wenu asipokuja pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kisha ulisema kwa watumishi wako ya kwamba hadi pale ndugu yetu mdogo aje pamoja nasi, hatutaweza kukuona tena"

Na ukawaambia watumishi wako

Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. "Kisha ukasema kwetu, watumishi wako"

asipokuja ... kushuka

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.

hamtauona uso wangu tena

Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. "Hamtaniona tena"

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

tulipokwenda kwa mtumishi wako baba yangu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kwenda" kuzungumzia safari kutoka Misri kwenda Kaanani.

tulimwambia maneno ya bwana wangu

Yuda anamtambua Yusufu kama "bwana wangu". Pia "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. "tulimwambia ulichosema, bwana wangu"

Na baba yetu akasema, Nendeni tena, mkatununulie chakula

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Baba yetu alituambia kurudi tena Misri kununua chakula kwa ajili yetu na familia zetu"

Nasi tukasema, "Hatuwezi kushuka. Ikiwa mdogo wetu ... pamoja nasi,

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kisha tukamwambia ya kwamba hatuwezi kushuka Misri. Tulimwambia ya kwamba iwapo ndugu yetu mdogo atakuwa pamoja nasi ... pamoja nasi"

kuuona uso wa mtu

Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. "kumuona yule mtu"