sw_tn/gen/44/18.md

1.5 KiB

alipomkaribia

"akakaribia"

mwache mtumishi wako

Yuda anajitambulisha kama "mtumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza kwa mtu mwenye mamlaka zaidi. Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "niruhusu mimi, mtumishi wako"

aseme neno katika masikio ya bwana wangu

Hapa "neno" ni lugha nyingine yenye maana ya kile kilichosemwa. Na "masikio" ni lugha nyingine yenye maana ya mtu mzima. "kuzungumza na wewe, bwana wangu"

masikio ya bwana wangu

Hapa "bwana wangu" ina maana ya Yusufu. Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "kwako"

na usiziache hasira zako kuwaka dhidi ya mtumishi wako

Kuwa na hasira inazungumzwa kana kwamba ilikuwa moto unawaka. "tafadhali usiwe na hasira na mimi, mtumishi wako"

kwani wewe ni kama Farao

Yuda anamlinganisha bwana yule na Farao kusisitiza nguvu kubwa ambayo bwana yule alikuwa naye. Pia anadokeza ya kwamba hakutaka bwana kuwa na hasira na kumuadhibu. "kwa maana wewe kama Farao mwenye mamlaka na unaweza kuwaamuru askari wako kuniua"

Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, kusema, Je mnaye baba au ndugu?'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Bwana wangu alituuliza kama tuna baba na ndugu"

Bwana wangu aliwauliza watumishi wake

Yuda anamtambua Yusufu kwa maneno haya "bwana wangu" na "wake". Pia anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wake". "Wewe, bwana wangu, alituuliza, watumishi wako" au "Ulituuliza"