sw_tn/gen/44/16.md

1.5 KiB

Je tunaweza kumwambia nini bwana wangu? Tuseme nini? au ni jinsi gani twaweza kujithibitisha wenyewe?

Maswali yote 3 yana maana moja. Wanatumia maswali haya kuweka msisitizo ya kwamba hakuna kitu wanaweza kusema kuelezea kilichotokea. "Hatuna kitu cha kusema, bwana wangu. Hatuwezi kuzungumza jambo lolote la maana. Hatuwezi kujithibitisha"

Je tunaweza kumwambia nini bwana wangu ... watumwa wa bwana wangu

Hapa "bwana wangu" ina maana ya Yusufu. Hii njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "Tunaweza kusema nini kwako ... watumwa wako"

Mungu ameona uovu wa watumishi wako

Hapa "ameona" haimaanishi Mungu ameona tu kile ndugu walichofanya. Ina maana Mungu sasa anawaadhibu kwa kile walichofanya. "Mungu anatuadhibu kwa dhambi zetu za zamani"

uovu wa watumishi wako

Ndugu wanajitambulisha wenyewe kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "dhambi zetu"

na yule ambaye kikombe kimeonekana mkononi mwake

Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. Pia, "kimeonekana" inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "na yule ambaye alikuwa na kikombe"

Na iwe mbali nami kwamba naweza kufanya hivyo

Kitu ambacho mtu hawezi kufanya inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu mtu anataka kuweka mbali na yeye. "sio kawaida yangu kufanya jambo kama hili"

Mtu ambaye kikombe kimeonekana mkononi mwake

Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. Pia, "kimeonekana" inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "mtu aliyekuwa na kikombe changu"