sw_tn/gen/42/29.md

796 B

bwana wa nchi

"bwana wa Misri"

aliongea nasi kwa ukali

"aliongea kwa jazba"

kuwa wapelelezi

Wapelelezi ni watu ambao kwa siri hujaribu kupata taarifa kuhusu nchi ili kuisaidia nchi nyingine.

Tukamwambia, 'Tu watu wa kweli sisi. Sisi siyo wapelelezi. Tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu. Mmoja hayupo hai tena ... nchi ya Kanaani

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Tulimwambia ya kwamba sisi ni watu waaminifu na sio wapelelezi. Tulisema kwamba tu ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu, na kwamba ndugu yetu hayupo hai tena ... nchi ya Kaanani"

Mmoja hayupo hai tena

Neno "ndugu" linaeleweka. "Ndugu mmoja hayupo hai tena"

mdogo yupo na baba yetu

Neno "ndugu" linaeleweka. "ndugu yetu mdogo yupo na baba yetu kwa sasa"