sw_tn/gen/39/03.md

975 B

Bwana wake akaona kwamba Yahwe alikuwa pamoja naye

Hii ina maana ya kwamba bwana wake aliona jinsi Yahwe alivyokuwa akimsaidia Yusufu. "Bwana wake aliona ya kwamba Yahwe alikuwa akimsaidia Yusufu"

kwamba Yahwe alifanikisha kila kitu alichokifanya

"Yahwe alisababisha kila kitu alichofanya Yusufu kufanikiwa"

Yusufu akapata kibali machoni pake

"Kupata kibali" ina maana ya kukubalika na mtu. Nomino ya "machoni pake" ina maana ya maoni ya mtu. Maana zaweza kuwa 1) "Potifa alifurahishwa na Yusufu" au 2) "Yahwe alifurahishwa na Yusufu"

Akamtumikia Potifa

Hii ina maana ya kwamba alikuwa mtumishi wa binafsi wa Potifa.

Potifa akamfanya msimamizi juu ya nyumba yake, na kila alichokimiliki

"Potifa alimweka Yusufu kusimamia nyumba yake na kila kitu kilichokuwa cha Potifa"

akakiweka chini ya uangalizi wake

Pale ambapo kitu "kinakuwa chini ya uangalizi wa mtu" ina maana ya kwamba mtu anawajibika na utunzanji na uhifadhi wake. "alimfanya Yusufu kutunza"