sw_tn/gen/38/24.md

964 B

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Yuda akaambiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu akamwambia Yuda"

Tamari mkweo

mkweo - "Tamari, mke wa mwana wako mkubwa"

yeye ni mjamzito kwa tendo hilo

Hapa neno la "hilo" lina maana ya "ukahaba" alioufanya. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "limemfanya aweze kuwa na mimba" au "ana mimba"

Mleteni hapa

"Mleteni nje"

ili achomwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "tutamchoma mpaka kufa"

Alipoletwa nje

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walipomleta nje"

mkwewe

mkwewe - "baba wa mume wake"

mhuri huu na mshipi na fimbo

"Mhuri" ni sawa na sarafu yenye mchoro uliochongwa juu yake, unaotumika kuchapa nta iliyoyeyushwa. "Mshipi" uliwekwa katika mhuri ili kwamba mmiliki angeweza kuvaa shingoni mwake. Fimbo ilikuwa mti mrefu wa mbao uliosaidia kutembea juu ya ardhi ngumu.

Shela

Haya ni majina ya wana wa Yuda.