sw_tn/gen/35/04.md

1.2 KiB

Hivyo wakampa

"kwa hiyo kila mmoja katika nyumba ya Yakobo akatoa" au "kwa hiyo kila mtu katika familia na watumishi walitoa"

iliyokuwa mikononi mwao

Hapa "mikononi mwao" ina maana ya kile walichomiliki. "kilichokuwa mali yao" au "walivyokua navyo"

heleni zilizokuwa katika masikio yao

"heleni zao". Maana zaweza kuwa 1) dhahabu katika heleni zingeweza kutumika sanamu zingine au 2) walichukua heleni hizi kutoka kwenye mji wa Shekemu baada ya kuishambulia na kuwaua watu wote. Heleni zingewakumbusha juu ya dhambi yao.

Mungu akaifanya miji yote iliyokuwa karibu nao kuhofu

Mungu kusababisha watu wa miji kumuogopa Yakobo na familia yake inazungumziwa kana kwamba "hofu" ilikuwa kitu kilichoanguka juu ya miji. Nomino inayojitegemea "hofu" inaweza kuwekwa kama "kuogopa". "Mungu aliwafanya watu waliozunguka miji kumuogopa Yakobo na wote aliokuwa nao"

miji yote

Hapa "miji" ina maana ya watu wanaoishi katika miji.

wana wa Yakobo

Inasemekana ya kwamba hakuna mtu aliyeshambulia familia ya Yakobo. Lakini wana wawili, Simoni na Lawi walishambulia ndugu wa Wakaanani wa Shekemu baada ya kumkamata na kulala na binti wa Yakobo. Yakobo aliogopa wangelipiza kisasi katika 34:30. "Familia ya Yakobo" au "Nyumba ya Yakobo"