sw_tn/gen/28/14.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Yakobo ndotoni.

Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi

Mungu analinganisha uzao wa Yakobo na vumbi la ardhi kuweka msisitizo ya idadi kubwa. "Utakuwa na uzao mkubwa zaidi ya utakavyoweza kuhesabu"

na utaenea mbali kuelekea magharibi

Hapa neno "utaenea" lipo katika hali ya upekee lakina lina maana ya uzao wa Yakobo. Inazungumzia kuhusu Yakobo kwa maana yeye ni kiongozi wa familia. "na uzao wako utasambaa hadi magharibi"

na utaenea mbali

Hii ina maana ya watu wataongeza mipaka ya ardhi yao na kukaa

katika maeneo makubwa zaidi.

kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini Misemo hii inatumika pamoja kumaanisha "pande zote". "katika pande zote"

Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitabariki familia zote juu ya dunia kupitia kwako na uzao wako"

Tazama

Hii inaongeza msisitizo kwa kile kinachosemwa baadae. "Tazama" au "Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachotaka kukuambia"

kwani sitakuacha. Nitafanya kila

"kwa kuwa sitakuacha mpaka nitende yote"

nitakulinda

"Nitakuweka salama" au "Nitakulinda"

Nitakurudisha katika nchi hii tena

"Nitakuleta katika nchi hii"