sw_tn/gen/26/15.md

905 B

Basi

Hapa neno hili halimaanishi "katika kipindi hiki". Inaonyesha wapi matukio ya simulizi yanapoanzia. Inaweza kutafsiriwa kwa neno unganishi "Kwa hiyo" kuonyesha ya kwamba hii ni tokeo la kilichotokea katika 26:12.

katika siku za Ibrahimu baba yake

Msemo wa "katika siku za" ina maana ya maisha ya mtu. "wakati Abrahamu, baba yake, alipokuwa akiishi"

Abimeleki akamwambia

Maana zaweza kuwa 1) hili ni tukio lingine kumlazimisha Isaka na watu wake kuondoka. "Kisha Abimeleki akasema" au "Hatimaye Abimeleki akasema" au 2) Abimeleki alifanya uamuzi huu kwa sababu aliona ya kwamba watu wake walikuwa na wivu na walitenda uhasama dhidi ya Isaka. "Basi Abimeleki akasema"

nguvu kuliko sisi

"mwenye nguvu zaidi ya sisi"

Hivyo Isaka akaondoka

Isaka pekee ametajwa kwa sababu yeye ni kiongozi, lakini familia yake na watumishi wake walienda naye. "Kwa hiyo Isaka na nyumba yake waliondoka"