sw_tn/gen/25/07.md

914 B

Hizi ndizo zilikuwa siku za miaka ya uhai wake Abrahamu alizoishi, miaka 175

"Abrahamu aliishi miaka 175"

Abrahamu akapumua pumzi ya mwisho na akafa

"Abrahamu alivuta pumzi yake ya mwisho na akafa". Misemo ya "alivuta pumzi ya mwisho" na "akafa" ina maana ya kitu kimoja. "Abrahamu alikufa"

akapumua pumzi ya mwisho

Hii ni njia ya upole ya kusema mtu alikufa.

katika uzee mwema, mzee aliye shiba siku

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Abrahamu aliishi muda mrefu sana. "alipomaliza kuishi muda mrefu na akawa mzee sana"

mzee aliye shiba siku

Kuishi maisha marefu sana inazungumzwa kana kwamba maisha yalikuwa chombo kinachoweza kujaa.

akakusanywa kwa watu wake

Hii ina maana ya kwamba Abrahamu alikufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "aliwaunga familia yake ambao walikuwa wameshakufa"