sw_tn/gen/24/39.md

1.5 KiB

Taarifa ya Jumla:

Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.

pengine mwanamke huyo asikubali kufuatana nami

Hili ni jambo ambalo linaweza kutokea. "Je kama mwanamke hatakuja pamoja nami" au "Nitafanyaje iwapo mwanamke huyu hatakuja pamoja nami?"

mbaye ninakwenda mbele yake

Kumtumikia Yahwe inazungumzwa kana kwamba Abrahamu alikuwa akitembea ndani ya uwepo wa Yahwe. "ambaye namtumikia"

atakufanikisha njia yako

"atafanya safari yako kufanikiwa"

ukoo wa baba yangu

"familia"

Lakini utakuwa huru katika kiapo changu ikiwa utafika kwa ndugu zangu na wasikuruhusu kuja naye. Ndipo utakuwa huru katika kiapo changu

Hii ni nadharia tete ambayo Abrahamu alifikiri isingeweza kutokea. Maana zaweza kuwa 1) "Kuna njia moja tu ya kuwa huru na kiapo changu: iwapo utakuja kwa ndugu zangu na hawatakupatia mwanamke kwako, basi utakuwa huru kutoka kwa kiapo changu" au 2) kujengea mstari wa 40, "iwapo utaenda kwa familia ya baba yangu na kumuuliza msichana, utakuwa umefanya kile nilichokuomba ufanye. Iwapo hawatakupatia msichana kwako, basi utakuwa huru kwa kipao ulichoapa kwangu"

Lakini utakuwa huru katika kiapo changu

"utafunguliwa kutoka kwa kiapo ulichofanya kwangu". Kushindwa kutimiza kiapo inazungumzwa kana kwamba mtu yupo huru na kitu kilichomfunga. "hautapaswa kufanya kile ulichoapa kwangu ambacho ungefanya"

ikiwa utafika kwa ndugu zangu

Lugha zinatumia maneno "njoo" na "kwenda" tofauti. "iwapo utafika kwa nyumba ya ndugu zangu" au "utakapokwenda kwa ndugu zangu"