sw_tn/gen/24/12.md

1.7 KiB

Kisha akasema

"Kisha mtumishi akasema"

anijalie kufanikiwa leo na aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abrahamu

Unaweza kuiweka hii kwa neno kiunganishi "kwa". Hii inaonyesha kwa uwazi jinsi mtumishi anataka Mungu amuonyeshe uaminifu wake. "Onyesha agano la uaminifu kwa bwana wangu Abrahamu kwa kunipatia mafanikio leo"

anijalie kufanikiwa

"nipatie mafanikio". Mtumishi alitaka kupata mke mwema kwa mwana wa Abrahamu. Nomino inayojitegemea ya "mafanikio" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "nisaidie nifanikiwe" au "nifanye niweze kufanya kile nilichokuja kukifanya"

aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abrahamu

Huu ni uaminifu kwa sababu ya agano ambalo Mungu alifanya na Abrahamu. Nomino inayojitegemea ya "uaminifu" inaweza kuelezwa "uwe mwaminifu". "Uwe mwaminifu kwa bwana wangu Abrahamu kwa sababu ya agano lako"

Tazama

Hapa neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

chemchemi ya maji

"chemichemi" au "kisima"

binti za watu wa mji

"wanawake vijana wa mji ule"

Na itokee kama hivi

"Na itokee kwa namna hii" au "Fanya hii ifanyike"

Nikimwambia msichana, 'tafadhari tua mtungi wako ili niweze kunywa maji,'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Hii inaweza kuelezwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Ninapomuuliza msichana aniruhusu kunywa maji kutoka kwenye mtungi wake"

tafadhari tua mtungi wako

Wanawake walibeba mitungi juu ya mabega yao. Alitakiwa kushusha na kumpatia mwanamume anywe.

mtungi

chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.

kuwa umeonesha agano la uaminifu kwa bwana wangu

Nomino inayojitegemea "uaminifu" inawezakuelezwa kama "alikuwa mwaminifu". "ya kwamba ulikuwa mwaminifu kwa bwana wangu kwa sababu ya agano lako"