sw_tn/gen/22/15.md

2.1 KiB

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

mara ya pili

Neno "pili" ni namba ya mpango kwa ajili ya mbili

kutoka mbinguni

Hapa neno "mbinguni" lina maana ya sehemu anapoishi Mungu.

na kusema - Hiki ni kiapo cha Yahwe

"na kuzungumza ujumbe huu kutoka kwa Yahwe" au "na kutamka maneno haya ya Yahwe". Hii ni njia ya fasaha ya kusema ya kwamba maneno yanayofuata yanatoka moja kwa moja kwa Yahwe.

Kwa ajili ya nafsi yangu nimeapa

"Nimeahidi na mimi ni shahidi wangu mwenyewe". Msemo "kuapa kwa" una maana kutumia jina la kitu au mtu kama msingi au nguvu ambayo kiapo kinafanyika. Hakuna kitu chenye nguvu zaidi ya Yahwe kuapa kwa jina lake mwenyewe.

umefanya jambo hili

"umenitii"

hukunizuilia mwanao

"hukumzuia nyuma mtoto wako wa kiume". Hii inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "ulikuwa tayari kumtoa mwanao kwangu"

mwanao, mwanao wa pekee

Inaonyesha ya kwamba Mungu anajua ya kuwa Abrahamu ana mtoto mwingine, Ishmaeli. Hii inasisitiza ya kwamba Isaka ni mwana ambaye Mungu alimuahidi kumpatia Abrahamu.

hakika nitakubariki

"hakika nitabariki"

nitakuzidishia uzao wako

Nitasababisha uzao wako kuongezeka tena na tena" au "Nitasababisha uzao wako kuwa mwingi"

kama nyota za angani, na kama mchanga ulioko kwenye ufukwe wa bahari

Mungu alifananisha uzao wa Abrahamu na nyota na mchanga. Kama vile watu wasivyoweza kuhesabu idadi kubwa ya nyota au chembe za mchanga, kwa hiyo kutakuwa na uzao mwingi wa Abrahamu ambao watu wasingeweza kuwahesabu. "zaidi ya kile uwezavyo kuhesabu"

kama nyota za angani

Hapa neno "mbinguni" ina maana ya kila kitu tunachoona juu ya dunia, kujumlisha jua, mwezi na nyota.

watamiliki lango la adui zao

Hapa "lango" linawakilisha mji wote. "Kumiliki lango la adui zake" ina maana ya kuangamiza adui zake. "atawashinda adui zake kabisa"