sw_tn/gen/22/11.md

1.5 KiB

malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

kutoka mbinguni

Hii ina maana ya sehemu ambapo Yahwe anaishi.

Mimi hapa

"Ndio,ninasikiliza" au "Ndio, kuna nini?"

usinyooshe mkono wako juu ya kijana, wala usifanye jambo lolote kumdhuru

Msemo "usinyooshe mkono wako juu ya" ni namna ya kusema "usimdhuru". Mungu alisema kitu kile kile mara mbili kusisitiza ya kwamba Abrahamu hakupaswa kumdhuru Isaka. "usimdhuru kijana kwa njia yoyote ile"

sasa najua ... kwa ajili yangu

Maneno "najua" na "yangu" yana maana ya Yahwe. Unapotafsiri kilichomo ndani ya nukuu, sema kwa namna ambayo Yahwe alitumia maneno ya "najua" na "yangu" alipomaanisha Yahwe.

unamcha Mungu

Hii ina maana ya kumheshimu Mungu kwa undani na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii yeye.

kuona

"kwa sababu ninaona"

hukumzuilia mwanao ... kwa ajili yangu

"haujamshikilia nyuma mwanao ... kwangu" Hii inaweza kusemwa kwa njia ya chanya. "ulikuwa tayari kumtoa mwanao ... kwangu"

mwanao, mwanao wa pekee

Inasemekana ya kwamba Mungu anajua ya kuwa Abrahamu ana mtoto mwingine, Ishmaeli. Hii inasisitiza ya kwamba Isaka ni mwana ambaye Mungu alimuahidi kumpa Abrahamu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "mwana wako wa pekee ambaye nilikuahidi"