sw_tn/gen/22/01.md

1016 B

Ikawa kwamba

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

baada ya mambo hayo

Msemo huu una maana ya matukio katika sura ya 21.

Mungu akampima Abrahamu

Inasemekana Mungu alimpima Abrahamu kujifunza kama Abrahamu atakuwa mwaminifu kwake. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. Mungu alipima uaminifu wa Abrahamu.

Mimi hapa

"Ndio, nasikiliza" au "Ndio, kuna nini?"

mwanao wa pekee

Inasemekana ya kwamba Mungu anajua ya kuwa Abrahamu ana mtoto mwingine, Ishmaeli. Hii inasisitiza ya kwamba Isaka ni mwana ambaye Mungu alimuahidi kumpa Abrahamu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "mwana wako wa pekee ambaye nilikuahidi"

umpendaye

Hii inasisitiza upendo wa Abrahamu kwa mwanawe, Isaka.

nchi ya Moria

"nchi inayoitwa Moria"

akatandika punda wake

"akambebesha punda wake" au "akaweka juu ya punda kile kilichohitajika kwa ajili ya safari"

vijana wake

"watumishi"

kisha akapanga safari

"alianza safari yake" au "alianza kusafiri"