sw_tn/gen/21/12.md

765 B

Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako

"Usifadhaike kuhusu mvulana na mjakazi wako"

Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili

Hapa "maneno" yana maana ya kile kinachosemwa. "Fanya kila kitu ambacho Sara anakuambia kuhusu wao"

itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa

Msemo "utaitwa" una maana ya wale watakaozaliwa kupitia Isaka ndio wale Mungu anawatambua kuwa uzao ambao alimuahidi Abrahamu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Isaka ndiye atakayekuwa baba wa uzao niliokuahidi kwako"

Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa

Neno "taifa" lina maana ya Mungu atampatia uzao mwingi ili kwamba wawe taifa kubwa la watu. "Nitamfanya mwana wa mwanamke mjakazi pia awe baba wa taifa kubwa"