sw_tn/gen/20/08.md

997 B

Akawasimulia mambo haya yote

"Aliwaambia kila kitu ambacho Mungu alimwambia"

Umetufanyia jambo gani?

Abimeleki alitumia swali hili la balagha kumshtaki Abrahamu. "Umefanya jambo hili baya kwetu!" au "Tazama ulichokifanya kwetu!"

Umetufanyia

Neno "umetufanyia" hapa linajitegemea na halimhusu Abrahamu na Sara.

Ni kwa jinsi gani nimekutenda dhambi kwamba umeniletea ... dhambi?

Abimeleki alitumia swali hili la balagha kumkumbusha Abrahamu ya kwamba hakufanya dhambi dhidi ya Abrahamu. "Sijafanya jambo dhidi yako kusababisha wewe ulete ... dhambi."

kwamba umeniletea mimi na ufalme wangu dhambi hii kubwa

Kumsababishia mtu awe na hatia ya kutenda dhambi inazungumzwa kana kwamba "dhambi" ilikuwa jambo linaloweza kuwekwa juu ya mtu. "ya kwamba umetufanya mimi na ufalme wangu kuwa na hatia kwa dhambi hii mbaya"

ufalme wangu

Hapa "ufalme" ina maana ya watu. "juu ya watu wa ufalme wangu"

Umenifanyia mimi jambo ambalo halipaswi kufanywa

"Usingefanya jambo hili kwangu"