sw_tn/gen/20/04.md

1.5 KiB

Basi ... hajamkaribia

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya kubadilisha kutoka kwenye simulizi kwenda kwa taarifa kuhusu Abimeleki.

Abimeleki alikuwa bado hajamkaribia

Hii ni njia ya upole ya kusema hakufanya ngono pamoja naye. "Abimeleki hakulala na Sara" au "Abimeleki hakumgusa Sara"

hata taifa lenye haki

Hapa "taifa" lina maana ya watu. Abimeleki ana wasiwasi ya kwamba Mungu atawaadhibu sio yeye tu, lakini watu wake pia. "hata watu wasio kuwa na hatia"

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?' Hata Sara mwenyewe alisema, 'ni kaka yangu.'

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Zinaweza kutajwa kwa nukuu isiyo dhahiri. "Je sio yeye mwenyewe aliyeniambia ya kwamba huyo ni dada yaek? Hata yeye mwenyewe alinimbia ya kwamba ni kaka yake"

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?

Abimeleki alitumia swali la balagha kumkumbusha Mungu juu ya jambo alilokuwa akilifahamu tayari. Hii inaweza kufanywa kuwa kauli. "Abrahamu mwenyewe aliniambia 'Huyu ni dada yangu'" au "Abrahamu alisema ya kwamba ni dada yake".

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, ...Hata Sara mwenyewe

Maneno "yeye mwenyewe" na "Sara mwenyewe" yanatumika kuweka msisitizo kuleta nadhiri kwa Abrahamu na Sara na kuwalaumu kwa kilichotokea.

Nimefanya hili katika uadilifu wa moyo wangu na katika mikono isiyo na hatia.

Hapa "moyo" una maana ya mawazo yake au nia zake. Pia "mikono" hapa ina maana ya matendo yake. "Nimefanya hili kwa nia njema na matendo mema" au "Nimefanya hivi bila mawazo au matendo ya uovu"