sw_tn/gen/18/24.md

1.5 KiB

Taarifa ya Jumla:

Abrahamu anaendelea kuzungumza na Yahwe

Huenda wakawepo

"Chukulia wakawepo"

Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?

Abrahamu alikuwa na tumaini ya kwamba Yahwe angesema, "Sitaikatalia mbali". "Nadhani hautaikatalia mbali. Badala yake, utaiacha kuiharibu sehemu kwa sababu ya watakatifu hamsini ambao wapo pale"

utawakatilia mbali

"kuingamiza". Abrahamu anazungumzia kuwaangamiza watu kana kwamba alifagia uchafu na ufagio. "kuangamiza watu waliokuwa wakiishi pale"

na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?

Abrahamu alikuwa akitumaini ya kwamba Mungu angesema, "Nitaacha kuangamiza sehemu kwa niaba ya watu watakatifu hamsini walioishi pale"

usiuache mji

"ruhusu watu waishi"

kwa ajili ya hao

"kwa sababu ya"

Hasha usifanye hivyo

"Sitapenda ufanye jambo kama hilo" au "Haupaswi kutaka kufanya jambo kama hilo"

hivyo, kuwauwa

"jambo kama hili kama kuwaua" au "jambo kama hilo, yaani, kuwaua"

watakatifu watendewe sawa na waovu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "unatakiwa kuwatendea watakatifu sawa sawa na waovu"

Je Mhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?

Abrahamu alitumia swali hili la balagha kusema kile alichotarajia Mungu kukifanya. "Mhukumu wa ulimwengu wote hakika atafanya kilicho haki" au "Kwa kuwa wewe ni Mhukumu wa ulimwengu wote, hakika utafanya lililo sahihi!"

Mhukumu

Mungu anasemwa kama mhukumu kwa sababu yeye ni mhukumu aliye kamilika ambaye hufanya maamuzi ya mwisho kuhusu mema na mabaya.