sw_tn/gen/18/03.md

960 B

Bwana

Hili ni jina la heshima. Maana zaweza kuwa 1) Abrahamu alijua ya kuwa mmoja wa wanamume hawa alikuwa Mungu au 2) Abrahamu alijua ya kwamba wanamume hawa walikuja kwa niaba ya Mungu.

machoni pako

Abrahamu anazungumza na mmoja wa wanamume.

usinipite

"tafadhali msiendelee kupita"

mtumishi wako

"mimi". Abrahamu ana maanisha yeye mwenyewe katika njia hii kuonyesha heshima kwa mgeni wake.

Naomba maji kidogo yaletwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Niruhusu nikuletee maji" au "Mtumishi wangu atakuletea maji"

maji kidogo ... chakula kidogo

"maji kidogo ... chakula kidogo." Kusema "kidogo" ilikuwa lugha ya upole ya kuonyesha ukarimu. Abrahamu angewapatia maji na chakula cha kutosha zaidi.

mnawe miguu yenu

Utamaduni huu uliwasaidia wasafiri waliochoka kujiburudisha baada ya kutembea umbali mrefu.

wenu ... mji...

Abrahamu anazungumza na wanamume wote watatu, kwa hiyo "wenu" na "mji..." ni katika hali ya wingi.