sw_tn/gen/17/17.md

902 B

akasema moyoni mwake

"akawaza mwenyewe" au "akasema mwenyewe kimya kimya"

Je yawezekana mtoto azaliwe kwa mwanaume ambaye ana umri wa miaka mia moja?

Abrahamu alitumia swali hili la balagha kwa sababu hakuamini ya kuwa hili lingeweza kutokea. "Hakika mwanamume mwenye umri wa miaka mia moja hawezi kuwa baba wa mtoto!"

Je Sara, ambaye ana umri wa miaka tisini anaweza kuzaa mwana?

Tena Abrahamu alitumia swali la balagha kwa sababu hakuamini ya kuwa hili lingeweza kutokea. msemo "ambaye ana umri wa miaka tisini" unasema kwa nini Abrahamu hakuamini ya kwamba Sarai hataweza kuzaa mtoto. "Sarai ana umri wa miaka tisini. Hakika hawezi kuzaa mtoto wa kiume!"

Lau Ishmaeli angeweza kuishi kabla yako!

"Tafadhali muache Ishmaeli arithi agano ulilofanya pamoja na mimi" au "Huenda Ishmaeli anaweza kupokea baraka ya agano lako" Abrahamu alipendekeza jambo ambalo aliamini lingeweza kutokea"