sw_tn/gen/16/11.md

1.1 KiB

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Sikiliza kwa makini"

utazaa mtoto kiume

"kuzaa mtoto wa kiume"

utamwita jina lake

"utamuita jina lake". Neno "utamuita" linamlenga Hajiri.

Ishmaeli, kwa sababu Yahwe amesikia

Watafsiri wanaweza kuweka maelezo mafupi yanayosema "Jina la 'Ishmaeli' lina maana ya 'Mungu amesikia'".

mateso

Alikuwa ameteswa na mawazo na mateso.

Atakuwa punda mwitu wa mtu

Hili halikuwa tusi. Inaweza kumaanisha Ishmaeli angekuwa anajitegemea na mwenye nguvu kama punda mwitu. "Atakuwa kama punda mwitu miongoni mwa watu"

Atakuwa adui dhidi ya kila mtu

"Atakuwa adui wa kila mtu"

kila mtu atakuwa adui yake

"Kila mtu atakua adui yake"

na ataishi kando na

Hii inaweza pia kumaanisha "ataishi kwa uadui pamoja na"

ndugu

"ndugu wa karibu"