sw_tn/gen/16/09.md

770 B

Malaika wa Yahwe akamwambia

"Malaika wa Yahwe alimwambia Hajiri"

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

bibi yako

Hapa ina maana ya Sarai. Bibi alikuwa na uwezo juu ya mtumwa wake. "mmiliki wake" au "Sarai"

Kisha Malaika wa Yahwe akamwambia, "Nita

Aliposema "Nita" alikuwa ana maana ya Yahwe.

Nitazidisha uzao wako maradufu

"Nitakupatia uzao mwingi sana"

wengi wasioweza kuhesabika

"wengi sana hadi hakuna mtu atakayeweza kuwahesabu"