sw_tn/gen/14/21.md

886 B

Nipatie watu

Msemo "watu" unaweza kuwa na maana ya watu wa Sodoma ambao maadui waliwakamata. Abramu aliwaokoa alipomuokoa Lutu.

Nimeinua juu mkono wangu

Hii ina maana "nimetoa kiapo" au "nimefanya ahadi".

Sitachukua chochote isipokuwa kile ambacho vijana wamekula

"Ninachukua kutoka kwako kile tu vijana wangu walishakwisha kula". Abramu alikuwa akikataa kupokea chochote kwa ajili yake, lakini alikiri kuwa wanajeshi wake wamekula sehemu ya akiba wakati wa safari ya kurudi Sodoma baada ya vita.

sehemu za watu waliokwenda nami.

Maana kamili ya kauli hii yawezwa kuwekwa wazi. "sehemu ya mali iliyokombolewa iliyokuwa ya wanamume walionisaidia kurudi"

Aneri, Eskoli, na Mamre

Hawa ni washirika wa Abramu (14:13). Kwa kuwa walikuwa washirika wa Abramu walipigana vita pamoja naye. Maana kamili ya kauli inaweza kufanywa wazi. "washirika wangu Aneri, Eskoli na Mamre"