sw_tn/gen/13/08.md

895 B

Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi,

"Tusigombane"

ugomvi

"chuki" au "ugomvi" au "malumbano"

na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu

"na tuwazuie wanaume wanaochunga wanyama wetu kulumbana"

licha ya hayo sisi ni familia

"kwa sababu sisi ni familia"

familia

"ndugu" au "jamaa". Lutu alikuwa mpwa wa Abramu.

Je nchi hii yote haiko mbele yako?

Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa katika hali ya chanya. "nchi nzima ipo wazi kwa matumizi yako"

Nenda na ujitenge na mimi

Abrahamu alizungumza kwa huruma na Lutu na kumtia moyo afanye jambo litakalowasaidia wote. "Tugawanyike".

Ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto

Maana zaweza kuwa 1) "ukienda njia moja, basi na mimi nitaenda njia nyingine" au 2) "ukienda kaskazini, nitaenda kusini." Abramu alimruhusu Lutu kuchagua sehemu ya nchi aliyoitaka, na Abramu angechukua kile kilichobaki.