sw_tn/gen/06/11.md

28 lines
957 B
Markdown

# Nchi
Maana yaweza kuwa 1) watu walioishi duniani au 2) "Dunia yenyewe"
# iliharibika
Watu waliokuwa wakifanya uovu inazungumziwa kana kwamba walikuwa chakula kilichooza. "ilioza" au "ilikua na ouvu sana"
# mbele za Mungu
Maana yaweza kuwa 1) "machoni pa Mungu" au 2) "katika uwepo wa Yahwe" kama 4:16.
# na ilijaa ghasia
Mwandishi anazungumzia ghasia kana kwamba ni kitu kinachoweza kuwekwa ndani ya chombo na nchi kama chombo. "na kulikuwa na wanadamu wenye vurugu sana nchini" au "kwa sababu ilikuwa imejaa watu waliofanya mambo maovu baina yao"
# tazama
Neno "tazama" hapa linatutahadharisha kuwa msikivu kwa taarifa ya kushtukiza inayofuata.
# wote wenye mwili
Maana yaweza kuwa 1) wanadamu wote au 2) viumbe vyote vyenye mwili, ikijumlisha wanadamu na wanyama.
# wameharibu njia zao
Namna mtu anavyoishi inazungumzwa kana kwamba ilikuwa njia au barabara. "waliacha kuishi kwa njia ambayo Mungu alitaka" au "waliishi katika njia ya uovu"