sw_tn/gen/06/01.md

901 B

Ikawa wakati

Msemo huu unatumika hapa kuonyesha alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

wana wa kike wakazaliwa kwao

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wanawake wakazaa mabinti"

wana wa Mungu

Haipo wazi kama hii inamaanisha viumbe wa mbinguni au wanadamu. Kwa vyovyote vile, walikuwa viumbe ambao Mungu aliumba. Baadhi wanaamini maneno haya yanamaanisha malaika waliomuasi Mungu, yaani, roho chafu au mapepo. Wengine wanadhani hii inamaanisha watawala wa kisiasa wenye nguvu, na wengine wanadhani hii inamaanisha uzao wa Sethi.

roho yangu

Hapa Yahwe anaongelea kuhusu yeye mwenyewe na roho wake, ambaye ni Roho wa Mungu.

nyama

Hii ina maana wana mwili ambayo itakufa siku moja

Wataishi miaka 120

Maana yaweza kuwa 1) urefu wa kawaida wa watu ingepungua hadi miaka 120. "Hawataishi zaidi ya miaka 120" au 2) katika miaka 120 kila mtu atakufa. "Wataishi miaka 120 tu"