sw_tn/gen/03/22.md

1.3 KiB

Mwanamume

Maana yaweza kuwa 1) Mungu alimaanisha binadamu mmoja, mwanamume au 2) Mungu alikuwa akimaanisha binadamu kwa ujumla, kwa hiyo ilimaanisha mwanamume na mke wake. Hata kama Mungu alikuwa akizungumza kuhusu mtu mmoja, alichosema kiliwahusu wote wawili.

kama mmoja wetu

"kama sisi". Kiwakilishi "sisi" ni wingi.

ajuaye mema na mabaya

Hapa "mema na mabaya" ni msemo ambao unamaana ya tofauti zote mbili na kila kitu katikati. "kujua kila kitu, ikiwemo mema na mabaya"

hataruhusiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Sitamruhusu"

mti wa uzima

"mti unaowapa watu uzima"

ardhi ambayo kwahiyo alikuwa ametwaliwa

"ardhi kwa maana alichukuliwa kutoka ardhini". Hii haimaanishi sehemu moja husika katika nchi ambayo Mungu alimchukua.

Kwa hiyo Mungu akamfukuza mtu huyu nje ya bustani

"Mungu alimlazimisha mwanamume aondoke bustanini." Hii inamaanisha tukio la 3:22, ambapo inasema "Yahwe Mungu alimfukuza kwenye bustani ya Edeni". Mungu hakumfukuza mwanamume mara ya pili.

kulima

Hii ina maana kinachohitajika ili mimea iweze kuota vizuri.

ili kulinda njia ya kwenda kwenye mti wa uzima.

"ili kuzuia watu wasiende kwenye mti wa uzima"

upanga wa moto

Maana yaweza kuwa 1) upanga ambao unatoa moto au 2) moto ulikuwa na umbo kama upanga.