sw_tn/gen/03/01.md

931 B

Sasa

Mwandishi anaanza sehemu mpya ya simulizi.

mwerevu kuliko

"mjanja zaidi" au "mwenye akili ya kupata kile atakacho kwa kusema uongo"

Je ni kweli Mungu amesema, 'Msile ... bustanini?

Nyoka anajifanya kushangazwa ya kwamba Mungu alitoa sheria hii. Swali hili la balagha laweza kutafsiriwa kama kauli. "Nashangaa ya kwamba Mungu, "Msile ... bustanini."

Msile

Neno "msile" ni wingi na linamaasha mwanamume na mwanamke

Twaweza kula ... Mungu amesema, 'msile'

Hawa alimwambia nyoka ambacho Mungu aliwaruhusu kufanya kwanza na kisha kile Mungu alichowazuia kufanya. Baadhi ya lugha zingesema kile walichozuiwa kufanya kwanza na kisha kusema kile walichoruhusiwa kufanya.

Twaweza kula

"Tunaruhusiwa kula" au "Tunayo ruhusa ya kula"

Msile ... wala ... mtakufa

Neno "msile" ni wingi na linamaasha mwanamume na mwanamke

Msile

"Hampaswi kula" au "Msile"

msiuguse

"na hampaswi kuigusa" au "na msiuguse"