sw_tn/gen/01/30.md

959 B

Taarifa ya jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza

kila ndege wa angani

"ndege wote wanaopaa angani"

chenye pumzi ya uhai

"kinachopumua". Msemo huu unasisitiza ya kwamba wanyama hawa walikuwa na uhai tofauti na mimea. Mimea haiwezi kupumua, na ilipaswa kutumika kama chakula cha wanyama. Hapa "uhai" una maana ya uhai wa mwili.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

Tazama

"hasa". Hapa neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata.

kikawa chema sana

Mungu alipotazama kila kitu alichokiumba, "kikawa chema sana".

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

siku ya sita

Hii inamaanisha siku ya sita ambapo ulimwengu ulianza kuwepo.