sw_tn/gen/01/26.md

1.3 KiB

na tufanye

Hapa neno "tumfanye" lina maana ya Mungu. Mungu alisema alichokusudia kukifanya. Kiwakilishi nomino "tu" ni wingi. Uwezekano wa sababu za wingi ni 1) wingi huu unaweza maanisha Mungu anajadili jambo na malaika ambao hukamilisha baraza lake la mbinguni au 2) wingi huu unaonyesha dalili baadae katika Agano Jipya kuhusisha ya kwamba Mungu yupo katika Utatu Mtakatifu. Baadhi hutafsiri kama "Na nifanye" au "Nitafanya". Kama utafanya hivi, basi zingatia kuweka maandishi mafupi kusema kuwa neno lina wingi.

mtu

"binadamu" au "watu". Neno hili hapa halimaanishi jinsia ya kiume pekee.

katika mfano wetu, wa kufanana na sisi

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza kuwa Mungu alifanya binadamu awe kama yeye. Mstari huu hausemi ni kwa njia zipi Mungu alifanya watu wawe kama yeye. Mungu hana mwili, kwa hiyo haimanishi watu watafanana na Mungu. "na kufanana na sisi".

wawe na mamlaka juu ya

"kutawala" au "kuwa na mamlaka juu"

Mungu akamuumba mtu ...alimuumba

Sentensi hizi mbili zina maana moja na zinasisitiza ya kwamba Mungu aliumba watu katika mfano wake.

Mungu akamuumba mtu

Namna Mungu alivyoumba binadamu ni tofauti na jinsi alivyoumba vitu vingine vyote. Usieleze bayana ya kwamba aliumba binadamu kwa kuongea, kama mistari ya nyuma inavyoonyesha.