sw_tn/gen/01/24.md

1.0 KiB

nchi na itoe viumbe hai

"Nchi na itoe vitu hai" au "na viumbe hai vingi viishi juu ya nchi". Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba nchi itoe viumbe hai, Mungu alifanya nchi itoe viumbe hai.

kila kiumbe kwa aina yake

"ili kwamba kila aina ya mnyama izae aina yake zaidi"

mnyama wa kufugwa, vitu vitambaavyo, na wanyama wa nchi

Hii inaonyesha ya kwamba Mungu aliumba kila aina ya wanyama. Iwapo lugha yako inayo namna nyingine ya kuunganisha wanyama wote katika kundi, basi waweza tumia hilo neno, au tumia kundi hili.

mnyama wa kufugwa

"wanyama wanaotunzwa na binadamu"

vitu vitambaavyo

"wanyama wadogo"

wanyama wa nchi

"wanyama mwitu" au "wanyama hatari"

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

Mungu akafanya wanyama wa nchi

"Kwa njia hii Mungu aliwafanya wanyama wa nchi"

Akaona kuwa ni vyema

Hapa "ni" inamaanisha viumbe hai wa nchi.