sw_tn/gen/01/20.md

957 B

Na maji yajae idadi kubwa ya viumbe hai

Hii ni amri. Kwa kuamuru viumbe hai wajaze maji, Mungu alifanya viwepo. Baadhi ya lugha huweza kuwa na neno moja linalomaanisha aina wote wa samaki na viumbe wa baharini. "Maji yajae viumbe wote" au "viumbe wengi wanao ogelea waishi baharini".

na ndege waruke

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba ndege waruke, Mungu alifanya waruke.

ndege

"wanyama warukao" au "vitu vinavyoruka"

anga tupu ya angani

"nafasi iliyo wazi ya angani" au "anga"

Mungu aliumba

"kwa njia hii Mungu aliumba"

viumbe wa majini wakubwa

"wanyama wakubwa wanaishi ndani ya bahari"

kwa aina yake

Vitu hai vya "aina" moja ni sawa na kule vilivyotokea.

kila ndege mwenye mabawa

"kila kitu kipaacho chenye mabawa." Iwapo neno kwa ajili ya ndege linatumika, linaweza kuwa kawaida kwa baadhi ya lugha kusema "kila ndege" kwa maana kila ndege ana mabawa.

Mungu akaona kuwa ni vyema

Hapa "ni" inamaanisha ndege na samaki.